Wednesday 5 April 2017

SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA YAAZISWA UPYA DAR



Watu waliokuwamo kwenye orodha ya kuhojiwa kuhusu dawa za kulevya na kutakiwa kufika Kituo Kikuu cha Polisi lakini hawakufika, wametakiwa kuripoti haraka. 

Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro bila kutaja idadi alisema jana miongoni mwao wamo walioorodheshwa kwenye orodha iliyokabidhiwa kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers Sianga. 

“Niwaombe wote waliopokea wito wa polisi waje wahojiwe kwa sababu mtu akija mwenyewe ni tofauti na akisubiri nguvu ya dola kutumika kumkamata,” alisema Siro.


No comments:

Post a Comment