Sunday 16 July 2017

VIDEO-TAZAMA GOLI LA HIMID MAO KWENYE MECHI YA STARS DHIDI YA RWANDA JANA


Leo Julai 15, 2017 imechezwa mechi kati ya Tanzania vs Rwanda kuwania kufuzu fainali za CHAN 2018 zitakazofanyika nchini Kenya, mechi hiyo imechezwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
Mechi imemalizika kwa sare ya kufungana goli 1-1, Rwanda walitangulia kufunga goli dakika ya 17 kipindi cha kwanza lililofungwa na Dominique Nshuti. Nahodha wa Stars Himid Mao Mkami akaisawazishia timu yake dakika ya 34 kipindi hichohicho cha kwanza.
Timu hizo zitarudiana tena Julai 23, 2017 nchini Rwanda mechi ambayo itaamua ni timu gani itasonga mbele katika harakati za kuwania kufuzu kucheza michuano ya CHAN.
Dauda TV inakuletea magoli yote pamoja na matukio mengine muhimu katika mechi hiyo.



No comments:

Post a Comment