Tuesday 14 February 2017

Baada ya mashabiki kumgomea Darassa kuachia wimbo mpya, sasa hiki ndicho walichoamua

Baada ya wimbo wa ‘Muziki’ kuwa ngoma ya kihistoria katika maisha ya Darassa kwa kumpatia heshima kubwa ndani na nje ya Tanzania, mashabiki wamemtaka kuachia wimbo mwingine mpya.

Japo mwezi Januari mwaka huu mashabiki hao walimgomea kuachia ngoma mpya huku wakimtaka kuendelea kusikilizia upepo wa ‘Muziki’ baada ya kuwauliza kupitia mtandao wa Instagram, kupitia mtandao huo mashabiki hao wamemtaka kuachia wimbo mpya baada ya kuwauliza kama wapo tayari afanye hivyo.
“Counting numbers before releasing a new hit!!!🔥…. Mpo tayariiiiiii AU bado bado ?,” Darassa ameandika kwenye Instagram.
Hizi ni baadhi ya comments za mashabiki wake kuhusu post hiyo:
director_ramymashy: Achia baba
spy_the_don_tz: Achia ki2, ucwape nafac ya kupumua………!
iam_najma: nimeskia nyimbo ya mziki kwenye super sport 2 wakati wa mchezo wa mashindando ya mchezo wa #longjump 😊😊😊😊🙌🙌🙌
r.a.y.m.a.r: Do more than musiki
wilsonhumphrey2002: Tayari tudondoshee zaidi ya muziki
youngtz1: Mzee baba kiwashe tu
27minjesha: Sasa tupo tayari..Achia mzinga huo wa nyuki!!
maasaisandles: Achia maana kukimbia tunaweza break zetu ziko vyema
gentilndoba: Tuko tayali @darassacmg all the love from Rwanda 🇷🇼.
luciorshandbag: Toa muzikiiioiiiiiiiiii acha maneno
sayprincechriz: Achia tuu iyo nyimbo ya taifa nyingne


No comments:

Post a Comment